Breaking News
recent

Iggy Azalea kurudi na album mpya...





























Msanii kutoka kwenye lebo ya T.I, Hustle Gang, Iggy Azalea amerudi tena kuziteka headlines kwenye kurasa za burudani… staa huyo mwenye asili ya Australia ametangaza kupitia page yake ya Twitter kuwa anarudi kwenye chati na album mpya alioipa jina ‘Digital Distortion’.
Kwenye page yake ya Twitter, Iggy Azalea aliwaambia mashabiki kuwa; “Digital Distortion sio jina la wimbo, ni jina la Album yangu”, tweet iliyokuwa inajibu swali la mmoja ya followers wake kwenye mtandao huo.
Iggy Iggz
Digital Distortion itakuwa album ya pili ya Iggy Azalea, Album yake ya kwanza The New Classic iliotoka mwaka jana na ilibeba nyimbo kama ‘Fancy’, ‘Black Widow’ nyimbo ambazo kwa mwaka 2014 zilibahatika kuchaguliwa kuwania tuzo za Grammy.
Iggy Iggz2
Kwenye Album hii mpya Iggy amefanya ngoma na baadhi wasanii ikiwemo Tinashe
iggy iggz3
Mipango yake kwa sasa ni kuachia single ya utangulizi iliyopewa jina ‘Zillion’ kabla ya kuachia single yake ya kwanza kutoka kwenye album yake mpya. Management ya Iggy Azalea imesema kuwa licha ye yeye kutoa single hizo mbili, Album yake itakuwa sokoni rasmi mwanzoni wa mwaka 2016.
ABC

ABC

No comments:

Post a Comment

Powered by Blogger.