Breaking News
recent

BBA The Chase: Baada ya kutolewa Betty akutana na vikwazo nchini kwake Ethiopia, hatarini kushitakiwa kwa “kufanya mapenzi hadharani” na Bolt!

Mtandao mmoja wa Ethiopia umeripoti kuwa aliyekuwa mshiriki wa nchi hiyo katika BBA ‘The Chase’ Betty Abera yuko hatarini kufunguliwa mashitaka kwa “kufanya mapenzi hadharani” na mpenzi wake Bolt katika reality show hiyo inayoendelea huko Afrika Kusini. Kwa mujibu wa mtandao wa Awramba Times wa Ethiopia, kikundi cha wanasheria wa Addis Ababa wamekamilisha maandalizi ya kumshitaki mshiriki huyo wa BBA ambaye tayari ameshauaga mchezo, kwa “kufanya mapenzi hadharani” kinyume cha sheria za nchi hiyo ambazo haziruhusu watu kufanya tendo hilo hadharani. Kwa mujibu wa radio moja ya Addis Ababa, endapo Betty atakutwa na hatia kuna uwezekano akatumikia kifungo cha miaka 6 nyuma ya nondo (jela). Inaaminika kuwa Bolt na Betty ndio walikuwa couple ya kwanza kufanya tendo hilo katika The Chase, kitu kilichoshuhudiwa na watazamaji wengi kutoka nchi mbalimbali za Africa . Baadhi ya watu wa Ethiopia wametoa maoni yao kwa kuonesha udhaifu wa tuhuma hizo kutokana na sababu kadhaa za msingi zikiwemo: 1.Betty hajafanya tendo hilo mbele za watu (public) kama inavyodaiwa kwasababu hapakuwa na mtu zaidi ya camera wakati tukio hilo likifanyika 2. Hakuna uthibitisho kama kweli walifanya tendo hilo sababu walikuwa wamejifunika blanketi 3. Tukio hilo halijafanyika ndani ya Ethiopia hivyo haina nguvu kwasababu sheria hiyo inafanya kazi ndani ya mipaka ya Ethiopia. 4. Serikali ya Ethiopia inapaswa kukishitaki kituo cha TV (DSTV) kilichorusha content hiyo kwa watazamaji wa Ethiopia na sio kumshitaki Betty.
ABC

ABC

No comments:

Post a Comment

Powered by Blogger.