Hakuna maana moja ya kumuelezea mwanaume, ila kwa aliye mwanaume
nadhani anaelewa nini maana ya kuitwa mwanaume, mara nyingi wanawake
huwa wanaonekana wao ndio wanaonewa sana na wanaume na ni vigumu sana
kujua manyanyaso ya wanaume sababu wengi huwa hawayaongelei, wanawake
wengi huwaongelea wanaume kwa ujumla yaani kuwafananisha wote katika
kundi moja. lakini kuna mtu na mtu kila mtu ana tabia zake na wanaume
wana tofautiana, sina maana ya kutetea haki za wanaume ila kuna fikira
potofu kuhusu wanaume ambazo watu wanatakiwa kuzitoa akilini.
Mwanaume halii
Mwanaume akionekana analia ataitwa dhaifu, ama hajakuwa bado mtoto,
lakini ukweli ni kwamba hata wanaume wana hisia wana umia na wana mioyo
kama wanawake, wao sio maroboti japokuwa inachukuliwa kuwa mwanaume
anayaeweza kuvumilia maumivu ndio jasiri bila kujua sio kila anaye lia
kwa machozi ni mnyonge. Kuna usemi wa mwandishi Malorie Blackman alisema
“Boys don’t cry, but men do.” katika kitabu chake cha Boys Don’t Cry.
Wanaume Wakorofi
Wapo wanawake wengi wameumizwa na vitendo vya kikatili kutoka kwa
wanaume zao, ndugu zao na marafiki, kupigwa na kuteswa na wanaume zao,
lakini si kweli wanaume wote wakorofi na wanadharau wanawake au watoto,
wapo wanaume wanaojali na kuheshimu wanawake pia.kuna mtu alisema
ukitaka kujua mwanaume mwenye hekima tazama heshima yake na mapenzi yake
kwa mama yake.
Wanaume hawafanyi Kazi za Nyumbani
Kazi za nyumbani sikuzote huonekana ni za wanawake tu,ni mara chache
usikie baba anaandaa chakula kwa ajili ya familia yake hata kama baba
huyo amesomea Mapishi na ana Degree, lakini wapo wanaume wanaosaidia
wake/wapenzi wao wakiwa nyumbani, kama ni kufua kupika na kuosha vyombo
wapo wanaojua nini maana ya kusaidia kazi za nyumbani.
Mwanaume ndiye Anaepanga Maamuzi juu ya Mwanamke
Sikataii wapo wanaume wa aina hii, wao wanapanga kila kitu, yeye ndo
atakwambia fanya hivi na usifanye hivi kitu ambacho si kila mwanaume
anafanya, wapo wanaojali maamuzi ya wenza wao na kuheshimu mambo yao,
tusiishi kwa mazoea.
Wanaume Wanapenda Michezo
Hapa sanasana mpira wa miguu, nilishangaa siku moja nilimuuliza mshikaji
mmoja anapenda timu gani ya mpira wa miguu alinijibu kirahisi tu ye si
mpenzi wa mpira wa mguu , nilishangaa lakini ukweli wapo wanaume ambao
sio wapenzi wa mpira wa miguu, ni kawaida kukutana na watu tofauti.
ABC
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment